VodaCom

Tangaza na gazeti la Bingwa.

NMB babu kubwa

Tangaza hapa huduma zako.

Commercial Bank of Africa

Tuna matumaini makubwa na huduma zako. Tangaza nasi.

AIRTEL huiweka dunia nzima karibu na watu

Haitoshi tu kusema AIRTEL YATOSHA. Inatosha kusema Airtel ni kila kitu.

TIGO, mtandao mkongwe zaidi nchini

TIGO ilionyesha njia. Sasa mawasiliano ni rahisi zaidi.

Sunday, November 10, 2013

Tambwe mguu ndani, nje Simba

NA ZAINAB IDDY


MSHAMBULIAJI wa Simba, Amisi Tambwe amesema hana muda mrefu kuitumikia Simba, kwani ameanza mazungumzo na timu moja ya Saudi Arabia.

Tambwe aliyasema hayo juzi kwenye mazungumzo maalumu saa chache kabla ya kuelekea Bujumbura, Burundi, baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara.

Alisema kuna uwezekano mkubwa akavunja mkataba na Simba na huenda asionekane katika kikosi hicho katika  mzunguko wa pili, endapo mazungumzo kati ya meneja wake, Alphonce George Twagilamungu yatakwenda  vizuri na timu hiyo ya Saudi Arabia.

“Kuna taarifa nimezipata kutoka kwa meneja wangu, kuna timu imevutiwa na kiwango changu kutoka Saudi Arabia, ila bado tupo kwenye mazungumzo,” alisema.

Tambwe alisema anataka kutumia muda huu wa mapunziko akiwa Burundi, kukutana na meneja wake ili kujua hatima ya uwepo wake Simba.

“Kazi yangu ni mpira, hivyo nipo tayari kucheza katika timu yoyote itakayonihitaji ili mradi timu husika ifuate taratibu za mahali nilipo na itimize yale ninayoyahitaji,” alisema.

Mrundi huyo alisajiliwa na Simba msimu huu kwa mkataba wa miaka miwili akitokea klabu ya Vital’O ya Burundi, ambapo ameonesha uwezo mkubwa katika mzunguko wa kwanza uliomalizika hivi karibuni.

Tambwe ni kinara wa upachikaji wa mabao Ligi Kuu Bara msimu huu, ambapo hadi mzunguko wa kwanza unamalizika, straika huyo ametikisa nyavu mara 10.

Vita kali ya usajili Simba, Yanga

NA ABDUCADO EMMANUEL

KITENDO cha Yanga SC kumsajili kipa wa zamani wa Simba SC, Juma Kaseja, kimeonesha kuamsha vita kali ya usajili miongoni mwa timu hizo, lengo likiwa ni kubomoana.

Kwa mujibu wa kalenda ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), inaonesha kuwa dirisha dogo la usajili litafunguliwa rasmi Ijumaa ijayo na kufungwa Desemba 15 mwaka huu.

Ijumaa iliyopita saa 2 usiku, Yanga ilifanikiwa kuinasa saini ya Kaseja, kwa dau la Sh milioni 40, kwa mkataba wa miaka miwili, ambapo waliwapiku wapinzani wao wa jadi Simba, ambayo nayo ilikuwa vitani kumwania.

Simba ilipanga kumrudisha kundini, Kaseja licha ya kumnyima mkataba mpya msimu huu, kutokana na kipa  Mganda, Abel Dhaira kuboronga kwa kufungwa mabao ya kizembe kwenye mechi mbalimbali alizoichezea timu hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani kutoka Simba, zinasema kuwa mara baada ya Kaseja kusajiliwa Yanga, klabu hiyo imekuwa na vikao vizito juzi na jana ambapo wametoka na azimio la kuibomoa klabu ya Yanga.

“Baada ya kumkosa Kaseja, hivi sasa tutapambana kumsajili kipa aliyekalia kuti kavu ndani ya Yanga, Ally Mustafa ‘Barthez’, ili kuimarisha nafasi ya kipa ambayo imepwaya,” kilisema chanzo hicho.

Simba inaweza kufanikiwa kwenye jaribio lake hilo, kutokana na Barthez kuwa mbioni kutimka Yanga, kufuatia kuandamwa na mashabiki mara kwa mara, baada ya matokeo ya sare ya mabao 3-3 dhidi ya Simba, wakidai alihujumu mechi hiyo na kuachia mabao kizembe.

Pia suala la kuwekwa benchi nalo linachangia kwenye mbio hizo za Barthez kutaka kuikacha Yanga, huku akiona giza zaidi mara baada ya kutua kwa Kaseja, kwani aliwahi pia kumkimbia akiwa Simba kutokana na kuwekwa kwake benchi.

“Kama hiyo (kumchukua Barthez) haitoshi, tumepanga kuibomoa Yanga kwa kuchukua mshambuliaji wao mmoja ambaye ni noma kwa kupachika mabao hivi sasa, ila hatuko tayari kutangaza kwa sasa,” kilizidi kueleza chanzo hicho

Katika kuhakikisha wamedhamiria kuitikisa Yanga, tayari wameingia kwenye vita ya kumwania kiungo wa timu ya Ruvu Shooting, Hassan Dilunga, ambaye pia anawaniwa na Wanajangwani.

Simba imepanga kumsajili ili kuziba pengo la Haruna Moshi ‘Boban’ aliyehamia Coastal Union msimu huu.

Mbali na majina hayo pia lipo jina la kiungo mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva, ambaye naye anateswa na mashabiki wa Yanga, ambao humzomea kila akiwa dimbani, hii ni kutokana na kutomwamini kinda huyo aliyetokea Ruvu Shooting, huku pia suala la kuwa na mapenzi na Simba likionesha kumtesa zaidi.

Hali kama hiyo inamkumba kiungo mshambuliaji wa Simba, Harun Chanongo, ambaye aliondoshwa kikosini mara baada ya kuboronga kwenye mechi dhidi ya Yanga, akihusishwa na mapenzi ya dhati aliyokuwa nayo kwa Yanga.

Ambapo inasemekana ni mmoja wa wachezaji aliyehusika kuihujumu Simba kwenye mechi hiyo, kufuatia kocha wa timu hiyo, Abdallah ‘King’ Kibadeni kukiri baadhi ya nyota wake kuhusika. Inaelezwa kuwa nyota huyo amepanga kutimkia Yanga ili kuondokana na hali hiyo inayoendelea kumtesa, baada ya kuwekwa kando kwenye kikosi cha Simba.

Hii si mara ya kwanza kwa Simba na Yanga, kuvurugiana mipango ya usajili pamoja na kubomoana vikosi vyao, kwani msimu uliopita Yanga iliibomoa Simba, kwa kumsajili beki wake kisiki Kelvin Yondani, huku Simba ikimsajili beki wa Yanga, Amir Maftah misimu miwili iliyopita.

Familia yampeleka Kaseja Yanga

NA EZEKIEL TENDWA

LICHA ya Juma Kaseja kuwa radhi kujiunga na timu yake ya zamani, Simba baada ya mzunguko wa kwanza kumalizika, kikwazo kikubwa kilikuwa kwa familia yake iliyomtaka kujiunga na Yanga.

Familia ya Kaseja ilifikia uamuzi huo baada ya Simba kumtema kipa huyo na nahodha ya timu ya Taifa, ‘Taifa Stars’ kabla ya msimu huu kuanza licha ya kuichezea kwa mafanikio makubwa tangu ajiunge nayo.

Tayari Kaseja amesaini mkataba wa miaka miwili Yanga baada ya benchi la ufundi kumpendekeza asajiliwe wakiamini ataiokoa timu hiyo katika michuano ya kimataifa inayowakabili, kutokana na kipa huyo kuwa na uzoefu mkubwa.

Kabla ya kusajiliwa na Yanga, viongozi wa Simba walitaka kumrudisha katika dirisha dogo lakini familia yake ilimsihi asirudi tena kwenye timu hiyo na badala yake aende kwa watani wao wa jadi Yanga hatua ambayo Kaseja aliitekeleza.

Simba ilimuacha Kaseja kwa madai ya kushuka kiwango, wakiwa na jeuri ya kumtumia, Abel Dhaira na Andrew Ntala ambao hata hivyo wameonekana kutokuwa makini kama Kaseja.

Hii ni mara ya pili Kaseja kusajiliwa na mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Bara, ambapo kabla ya hapo alishaichezea timu hiyo msimu 2008/09 na baadaye kurejea tena Simba.

Baada ya kusajiliwa na Yanga, Kaseja anaungana na magolikipa wawili wa timu hiyo, Ali Mustafa ‘Barthez’ pamoja na Deogratias Munish ‘Dida’ ambao wote wamewahi kuichezea Simba kabla ya kujiunga na Yanga.

Azam, Coastal Union watunishiana misuli

NA ZAITUNI KIBWANA

TIMU za Azam na Coastal Union zinazoshiriki michuano ya Kombe la Uhai inayoshirikisha wachezaji wenye umri chini ya miaka 20 wa klabu za Ligi Kuu, wametunishiana misuli kwenye michezo ya ufunguzi wa mashindano hayo.

Ofisa habari wa Azam, Jafari Iddi aliliambia BINGWA kuwa kikosi chao kimeahidi ubingwa wa michuano hiyo, hivyo Coastal Union wajiandae kwa kichapo.

Wakati Jafari akiyasema hayo msemaji wa Coastal Union, Hafidhi Kido alisema kuwa mwaka huu wana vijana watakaoleta changamoto kwenye michuano hiyo.

Michuano hiyo mwaka huu itafanyika kwenye viwanja vya Karume na Azam Complex, Dar es Salaam.

Kundi A linaundwa na timu za Azam, Coastal Union, JKT Ruvu Stars, Mbeya City na Yanga, wakati kundi B ni Ashanti United, Mgambo Shooting, Oljoro JKT na Ruvu Shooting, Kagera Sugar, Mtibwa Sugar, Rhino Rangers na Tanzania Prisons ndizo zinazounda kundi C.

Kwa mujibu wa Ofisa Mashindano, Idd Mshangama, alisema kuwa mechi hizo za ufunguzi timu za Yanga na Mbeya City (saa 8 mchana- Karume).

Kundi B ni Ruvu Shooting na Ashanti United saa 4 asubuhi- Karume, Oljoro JKT na Simba saa 10 jioni- Karume

Benchi la ufundi Simba kuwasilisha ripoti wiki hii

NA EZEKIEL TENDWA

RIPOTI ya benchi ya ufundi la timu ya Simba, inatarajiwa kuwasilishwa kwa  kamati ya utendaji wiki hii.

Akizungumza jana, Ofisa habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema kuwa makocha wa timu hiyo wameahidi kuwasilisha ripoti kwa kamati ya utendaji wiki ili iweze kufanyiwa kazi.

Alisema kwamba baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania bara na timu yao kumaliza wakiwa nafasi ya nne, walitoa muda kwa benchi lao la ufundi kuandaa ripoti hiyo ambayo wataiwasilisha ndani ya wiki hii.

“Baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza, tulitoa muda kwa benchi letu la ufundi kuandaa ripoti yao na mapendekezo yao ambapo ndani ya wiki hii wataiwasilisha nasi tutaifanyia kazi,” alisema.

Alisema baada ya kupata ripoti hiyo, wataifanyia kazi kwani lengo lao ni kuhakikisha mzunguko wa pili timu hiyo inafanya vizuri na kujikita kileleni mwa msimamo ambao kwa sasa unakaliwa na watani zao wa jadi Yanga.

Kocha Mgambo JKT alia na wachezaji

NA SALMA JUMA

KOCHA mkuu wa timu ya Mgambo JKT, Mohamed Kampira ameweka wazi sababu iliyopelekea timu yake kufanya vibaya katika mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara msimu huu, kuwa ni kuondoka kwa baadhi ya wachezaji wake aliokuwa nao katika ligi iliyopita.

Mgambo wanashikilia mkia kwenye msimamo wa ligi hiyo wakiwa na jumla ya pointi 6, baada ya kushinda mchezo mmoja, kutoka sare mechi tatu na kupoteza mechi 9.

Akizungumza na BINGWA hivi karibuni, Kampira alisema kuwa kubwa lililowaangusha  msimu huu hasa katika mzunguko wa kwanza uliomalizika Novemba 7 ni kupungua kwa baadhi ya wachezaji wake aliokuwa nao katika ligi iliyopita, lakini pia changamoto nyingi pamoja na ushindani wa hali ya juu kutoka katika kila timu.

Alisema kuwa kutokuwepo kwa wachezaji hao kumevuruga kabisa mfumo wake hasa katika safu ya ushambuliaji na ulinzi, kwani kikosi chake kimeonekana kupwaya sana katika maeneo hayo.

Kampira alisema kuwa kwa sasa anaandaa ripoti ya kuwakabidhi viongozi wa timu hiyo, ili kuangalia wachezaji wanaoweza kuongezwa katika nafasi hizo ili kikosi kiwe na uhai kwenye mzunguko wa pili wa ligi.

“Ni kweli tumefanya vibaya tena tofauti na msimu uliopita, na hali hiyo imechangiwa na kuondoka kwa baadhi ya wachezaji wangu niliokuwa nao msimu iliopita, lakini tutafanya marekebisho na kuongeza wachezaji kwani tumepoteza mechi nyingi na hatutarajii hilo lijirudie tena mzunguko wa pili na kubaki katika ligi hiyo mzunguko wa pili,” alisema.

Kung Fu Mbagala kufanya mashindano mara kwa mara

NA ZAINAB IDDY

UONGOZI wa klabu ya Kung Fu ya Mbangala jijini Dar es Salaam, umepanga programu ya kufanya mashindano ya mara kwa mara, kwa lengo la kuendeleza mchezo huo nchini.

Abdallah Nyoni ni Katibu Mkuu wa klabu hiyo, aliliambia BINGWA kwamba mashindano hayo yatasaidia kupata vipaji ambavyo vitawasaidia katika mashindano mbalimbali.

“Hiyo ni moja ya maandalizi ya kuwaandaa wachezaji kwa ajili ya mashindano mbalimbali mwakani, hivyo tunajipanga mapema,” alisema.

Alisema mwakani kutakuwa na mashindano mbalimbali ndani na nje ya nchi, ndiyo maana wameamua kutengeneza timu yao kupitia mashindano hayo.

Nyoni alisema mbali na programu hiyo, kutakuwa na mazoezi ya kila wiki ambayo yatawawezesha wachezaji kujiweka sawa na kuwa tayari muda wowote kushiriki michuano itakayoandaliwa na klabu nyingine.

“Tutahakikisha tunakuwa mfano wa kufanya vema katika mchezo huo nchini, ndiyo maana tunafanya mambo yote hayo,” alisema.

Sunday, August 4, 2013

Huruma ya kocha yaidhoofisha timu ya makanjanja



Timu ya taifa ya wasichana
KUCHELEWA kwa Bunge kupitisha Muswada wa Sheria ya Udhibiti wa Shughuli za Upangaji Nyumba na Makazi (Rental Housing Act), kunaipotezea Serikali mapato ya mabilioni ya fedha kuliko Sh 1000 ya kodi za kadi za simu (Simcard tax).

Akizungumza na MTANZANIA Jumatano, Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia, January Makamba, alisema ni vema sheria hiyo ikaanzishwa haraka ili kuondoa matatizo na lawama kuhusu kodi ndogo ndogo kama za kadi za simu zinazosumbua wananchi.

Makamba, alisema Wizara yake siyo iliyopanga tozo ya kodi hiyo kama baadhi ya wananchi wanavyodhani, kwa sababu haihusiki na kodi ya aina yoyote.

“Sheria ya udhibiti wa shughuli za upangaji, inatakiwa ije haraka kwani ndiyo hasa inayomnyonya mwananchi, kama unafanya kazi na unalipwa mshahara kwa mwezi, kwa nini ulipe kodi ya mwaka mzima, fedha ambayo haiendani na kipato.

“Kenya wanayo sheria hii ambapo mtu ana uwezo wa kulipia nyumba kwa miezi mitatu, kimataifa ni miezi miwili ambapo mtu analipia mwezi wa kwanza na wa mwisho.

“Sheria hii pia itasaidia kuanzishwa kwa mamlaka ya udhibiti wa nyumba kama ilivyo kwenye usafirishaji, ambako kuna Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), kwenye Nishati kuna EWURA, Chakula na Dawa kuna TFDA,” alisema.

Alisema malipo ya kodi ya nyumba kwa mwaka, ndiyo chanzo cha mtu kufanya maovu mengi kama kupokea rushwa, kujiingiza katika biashara ya dawa za kulevya, wizi na mengineyo.

Aidha, Makamba amesema Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, ni mnafiki kwa kukimbilia kutoa namba yake ya simu ya mkononi katika mkutano wa hadhara na kuandika kwenye mitandao, ili wananchi wampigie kumhoji kuhusu uwepo wa kodi kadi za simu wakati yeye mwenyewe alikuwepo bungeni kuipitisha.

“Mnyika ni mnafiki, yeye alikuwepo bungeni na alilijua fika suala hili wala hakusema kitu, baada ya kusikia watu wanalalamika ndiyo anaanza kuongea ongea.

“Ukiona mtu anafanya siasa nje ya Bunge ujue anatafuta umaarufu, kanuni zinamruhusu Mbunge yeyote kupeleka sheria ya mabadiliko, namna ya kubadilisha sheria sio kutoa namba za simu za watu, hizo ni siasa uchwara.

“Rais alishalitolea maamuzi na Serikali inalishughulikia, watu wasiwasikilize wanasiasa uchwara, wananchi wawe na subira kuhusu suala hili,” alisema Makamba.

Julai mwaka huu katika kikao chake cha bajeti, Bunge lilipitisha sheria ya kodi ya tozo ya kadi ya simu ya Sh 1000 kwa kila laini ya simu ya mkononi kwa mwezi, kodi ambayo imelalamikiwa na wananchi kuwa ni kubwa.

Hata hivyo, Rais Jakaya Kikwete, ameingilia kati suala hilo ambapo ameziagiza Wizara za Serikali zinazohusika na kodi na mawasiliano pamoja na kampuni za simu za mikononi nchini, kukutana mara moja kutafuta jinsi gani ya kumaliza mvutano wa kodi mpya ya kadi za simu hizo za mikononi.

Soka la Tanzania lapaa juu ya dari

Uwanja wa Sinza ukiwa katika hatua za mwisho

KUCHELEWA kwa Bunge kupitisha Muswada wa Sheria ya Udhibiti wa Shughuli za Upangaji Nyumba na Makazi (Rental Housing Act), kunaipotezea Serikali mapato ya mabilioni ya fedha kuliko Sh 1000 ya kodi za kadi za simu (Simcard tax).

Akizungumza na MTANZANIA Jumatano, Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia, January Makamba, alisema ni vema sheria hiyo ikaanzishwa haraka ili kuondoa matatizo na lawama kuhusu kodi ndogo ndogo kama za kadi za simu zinazosumbua wananchi.

Makamba, alisema Wizara yake siyo iliyopanga tozo ya kodi hiyo kama baadhi ya wananchi wanavyodhani, kwa sababu haihusiki na kodi ya aina yoyote.

“Sheria ya udhibiti wa shughuli za upangaji, inatakiwa ije haraka kwani ndiyo hasa inayomnyonya mwananchi, kama unafanya kazi na unalipwa mshahara kwa mwezi, kwa nini ulipe kodi ya mwaka mzima, fedha ambayo haiendani na kipato.

“Kenya wanayo sheria hii ambapo mtu ana uwezo wa kulipia nyumba kwa miezi mitatu, kimataifa ni miezi miwili ambapo mtu analipia mwezi wa kwanza na wa mwisho.

“Sheria hii pia itasaidia kuanzishwa kwa mamlaka ya udhibiti wa nyumba kama ilivyo kwenye usafirishaji, ambako kuna Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), kwenye Nishati kuna EWURA, Chakula na Dawa kuna TFDA,” alisema.

Alisema malipo ya kodi ya nyumba kwa mwaka, ndiyo chanzo cha mtu kufanya maovu mengi kama kupokea rushwa, kujiingiza katika biashara ya dawa za kulevya, wizi na mengineyo.

Aidha, Makamba amesema Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, ni mnafiki kwa kukimbilia kutoa namba yake ya simu ya mkononi katika mkutano wa hadhara na kuandika kwenye mitandao, ili wananchi wampigie kumhoji kuhusu uwepo wa kodi kadi za simu wakati yeye mwenyewe alikuwepo bungeni kuipitisha.

“Mnyika ni mnafiki, yeye alikuwepo bungeni na alilijua fika suala hili wala hakusema kitu, baada ya kusikia watu wanalalamika ndiyo anaanza kuongea ongea.

“Ukiona mtu anafanya siasa nje ya Bunge ujue anatafuta umaarufu, kanuni zinamruhusu Mbunge yeyote kupeleka sheria ya mabadiliko, namna ya kubadilisha sheria sio kutoa namba za simu za watu, hizo ni siasa uchwara.

“Rais alishalitolea maamuzi na Serikali inalishughulikia, watu wasiwasikilize wanasiasa uchwara, wananchi wawe na subira kuhusu suala hili,” alisema Makamba.

Julai mwaka huu katika kikao chake cha bajeti, Bunge lilipitisha sheria ya kodi ya tozo ya kadi ya simu ya Sh 1000 kwa kila laini ya simu ya mkononi kwa mwezi, kodi ambayo imelalamikiwa na wananchi kuwa ni kubwa.

Hata hivyo, Rais Jakaya Kikwete, ameingilia kati suala hilo ambapo ameziagiza Wizara za Serikali zinazohusika na kodi na mawasiliano pamoja na kampuni za simu za mikononi nchini, kukutana mara moja kutafuta jinsi gani ya kumaliza mvutano wa kodi mpya ya kadi za simu hizo za mikononi.

Utata mafuta ya ubuyu

Vita ya uwanjani imetimia

NA GABRIEL MUSHI
SIKU moja baada ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, kutoa tamko linaloeleza kuwa mafuta ya ubuyu hayana madhara katika mwili wa binadamu yakitumiwa vizuri, Serikali imekanusha hilo kwa kuwaonya wananchi wasiyatumie kwa sababu ni hatari.

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, jana alitangaza kuwa mafuta hayo si salama na kusisitiza kuwa huo ndiyo msimamo wa Serikali kuhusu mafuta hayo, hivyo wananchi waamue wenyewe kuyatumia au kutoyatumia.

Dk. Rashid alitoa kauli hiyo wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari baada ya kufungua semina ya siku mbili, iliyoandaliwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA) na Shirika la Afya Duniani (WHO).

Alisema kwa kuwa tayari TFDA imeshatoa tamko kuwa mafuta hayo si salama, hivyo wananchi ni hiari yao kutekeleza agizo hilo au kutolitekeleza.

“Tayari chombo cha serikali ambacho kina mamlaka juu ya hili kimeshatoa tamko, hivyo ni hiari ya wananchi kuamua wenyewe kuyatumia au kutoyatumia.

“Kwa sababu ni sawa na sigara, tumesema kabisa sigara inasababisha saratani na matatizo mengine tukaweka na onyo kwenye kasha la sigara zenyewe, hivyo ni hiari kutumia au kutotumia.

Alisema madhara yaliyo kwenye mafuta ya ubuyu yamegundulika hivi karibuni, baada ya kufanyiwa uchunguzi ambao ulichukua muda mrefu na hivyo kuchelewa kutangaza madhara yake.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Dk. Rashid, Mkurugenzi Mtendaji wa TFDA, Hiiti Sillo, alisema semina hiyo inashirikisha nchi 16 zilizopo kusini mwa Jangwa la Sahara.

Alisema imeandaliwa kwa ajili ya kuwapatia wakaguzi mbinu mpya za kudhibiti dawa bandia ambazo zinasababisha madhara kwa binadamu.

“Tatizo la dawa bandia linatakiwa kushirikiana na nchi nyingine, ndiyo maana mafunzo haya yatatumika kujenga uhusiano pamoja na kubadilisha uzoefu namna ya kukamata dawa hizo,” alisema.

Mwakilishi wa Shirika la Afya kutoka Geneva, Dk. Michael Deats, alisema tatizo la dawa bandia ni tatizo sugu linalozisumbua nchi za Bara la Afrika.

Hivi karibuni, TFDA ilipiga marufuku matumizi ya mafuta ya ubuyu kwa madai kuwa yanasababisha saratani, tamko ambalo lilipingwa vikali na wataalamu wa tiba mbadala.

Pamoja na hilo, juzi Taasisi ya Saratani ya Ocean Road  ilitangaza kuwa mafuta hayo ni salama iwapo yakitumiwa vizuri, tamko hilo pamoja na mwendelezo wa malalamiko kutoka kwa wananchi na wataalamu mbalimbali, limekuwa likizua utata kwa kuwa kila upande unaonekana kutoa msimamo wake jambo ambalo limeibua mjadala katika jamii.

Wabunge wagombea Sh milioni 1

Wakongwe wakijiandaa kwa kabumbu

NA JOHN MADUHU, MWANZA
WABUNGE wawili wa Kanda ya Ziwa, wameingia katika mzozo wa kugombea shilingi milioni moja.
Wabunge hao ni Lameck Airo wa Jimbo la Rorya mkoani Mara (CCM) na Ezekiel Wenje wa Jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza.

Akizungumza na MTANZANIA Jumatano jana kuhusu chanzo cha mzozo huo, Airo alisema anamtaka Wenje amrejeshee Sh milioni moja, alizompatia kwa ajili ya harambee ya kuchangia Shule ya Msingi ya Buchili wilayani Rorya, kwa sababu amezitumia badala ya kwenda kutoa mchango.

Airo alisema Wenje alikwenda kumuomba Sh milioni 5 mwishoni mwa wiki iliyopita alizodai kuwa ni mchango kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Buchili pamoja na ununuzi wa madawati na kumtaka ahudhurie harambee hiyo, lakini ratiba yake haikumruhusu hivyo alimpatia Sh milioni 1 ya mchango.

Alisema alishangazwa na taarifa alizopata kutoka kwenye harambee hiyo, kuwa Wenje hakutoa mchango aliompatia na badala yake alitoa maneno ya kashfa dhidi yake pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rorya, Charles Ochere, ambaye naye alimchangia kiasi cha Sh 500,000.

Alilalamika kuwa kitendo cha Wenje kutafuna fedha zake ni cha kihuni na kumtaka azirejeshe huku akimtahadharisha kuacha kumchafua katika majukwaa na badala yake washindane katika kuwaletea maendeleo wananchi.

“Nimempatia fedha kwa ajili ya harambee kiasi cha Sh milioni moja na Mwenyekiti naye alitoa Sh 500,000, kwanini hakutangaza mchango wetu katika harambee hiyo na badala yake yeye binafsi alitoa milioni moja pekee bila kutaja tulizompatia, inatia aibu kwa Mbunge kuchukua fedha kwa wabunge wenzako bila kuzifikisha kunakohitajika, kama alikuwa anataka kuongezea mtaji kwa ajili ya duka lake la madawa ni afadhali angetueleza,” alisema Airo.

Aidha Airo alieleza kusikitishwa na kauli iliyotolewa na Mbunge huyo katika harambee hiyo, kuwa amekuwa akimsaidia mambo kadhaa wakiwa bungeni mjini Dodoma na kueleza kuwa huo ni uongo.

Alipotafutwa Wenje kupitia simu yake ya kiganjani kuzungumzia tuhuma hizo, iliita bila kupokelewa.

Saturday, August 3, 2013

Hasheem Thabiti: Balozi wa kikapu nchini aliyekumbukwa na Obama

Na Markus Mpangala, Dar es Salaam
Hasheem alipokuja nchini mwake hivi karibuni
DIKEMBE Mutombo ni jina maarufu sana Afrika na duniani kote, kutokana na uwezo wake wa kucheza kikapu. Lakini jina lake kamili ni Dikembe Mutombo Mpolondo Mukamba Jean-Jacques Wamutombo.

Nyota huyo ana sifa kubwa kutokana na alivyoweza kusaidia ukuzaji wa mchezo huo, katika bara la Afrika hususani nchini mwake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mutombo kama anavyofahamika, alikuwa akicheza Ligi ya kulipwa ya Kikapu nchini Marekani, kwenye timu ya Houston Rockets. Kwa bara la Afrika mchezo wa Kikapu unapendwa zaidi kwenye nchi za Angola, Morocco na Nigeria pamoja na Tanzania, ambazo kwa nyakati tofauti zimekuwa na ufanisi kwa wachezaji wake.

Tunamkumbuka Mutombo kama tunavyofanya kwa Hasheem Thabiti, ambaye amekuwa akicheza Ligi ya Kulipwa ya Kikapu katika timu ya Oklahoma City Thunder ya Marekani.

Watanzania tunatakiwa kujivunia nyota huyo, ambaye amekuwa na mchango mkubwa wa maendeleo ya mchezo wa kikapu hapa nchini na kuonyesha kila dalili za kufuata nyayo za Dikembe Mutombo, ambaye aliisaidia sana nchi yake.

Bahati nzuri pia, ziara ya Rais Barack Obama, imefungua masikio ya wengi kuwa anatambua kuwa tunaye mchezaji mahiri nchini mwake. Katika mazungumzo yake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Rais Obama alisema kuwa anatambua kuwa nchi yetu inaye mchezaji kikapu, na hivyo kufanya mazungumzo ya kipekee na mwenyeji wake Rais Kikwete.

Kwa namna nyingine, kauli ya Rais Obama inatukumbusha kuwa kuna uwezekano mkubwa sana, sekta ya michezo hususani mchezo wa kikapu ikanufaika zaidi na matembezi yake ya kikazi.

Tunakumbuka kuwa klabu ya Seattle Sounder ya Marekani, ilimchukua winga Mrisho Ngassa wakati akichezea Azam, ili kufanya majaribio klabuni hapo.

Tuliona Ngassa akicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Manchester United. Tunafahamu kuwa Seattle Sounders iliingia ubia na klabu ya African Lyon ya hapa nchini, ili kuendeleza michezo, huku Azam nayo ikiwa mshirika mzuri.

Ziara ya Obama ambayo inamkumbuka nyota wetu Hasheem Thabiti, bila shaka inafungua milango zaidi kwa wachezaji wa mpira wa kikapu na sekta ya michezo kwa ujumla.

Rais Kikwete amekuwa na juhudi za kuendeleza michezo, tangu nia ya kuialika klabu ya Real Madrid, pamoja na mikakati ya sasa ya kuanzishwa akademi ambayo itaishirikisha klabu ya Sunderland ya England.

Ziara ya Obama na kutajwa kwa Hasheem Thabiti, kuna maana moja kuwa rais huyo anatambua kuwa Tanzania imejaliwa vipaji, ndiyo maana mchezaji huyo amekuwa miongoni mwa nyota waliosajiliwa na timu ya kulipwa za ligi ya NBA nchini Marekani.

Kuna kitu kimoja muhimu cha kukiangalia hapa, Obama ametembelea mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Symbion, ambayo ni mshirika wa klabu ya Sunderland.

Kwa maana hiyo ushirika huo kwa wanamichezo, utaleta manufaa makubwa, kwani kwenye mazungumzo yake Rais Obama ameeleza kutambua umuhimu wa Thabiti.

Bila shaka, juhudi zilizofanywa na Thabiti katika kuendeleza mchezo huu, na kwa kuwa alishawahi kukutana na Rais Kikwete mara kadhaa, sasa nyongeza itakuwepo na sekta ya michezo itapata mwamko mpya.

Ni rahisi kutumia ziara hii kuanzisha ushirikiano wa Sunderland, Symbion na Oklahoma City Thunder, ili kuupa kipaumbele mchezo wa kikapu kote nchini, ikiwezekana zaidi ya kipindi cha utawala wa Jackson Kalikumtima.

Tunafahamu tangu kuondoka kwa Jackson Kalikumtima, mchezo wa kikapu haukuwahi kupiga hatua kubwa, lakini kwa ziara ya Rais Obama, ni muhimu kwa wadau wa mchezo huo kusaka njia mbadala ya kuboresha zaidi.

Kwa hakika Thabiti ni balozi wetu wa mchezo wa kikapu, ambaye amekumbukwa na Rais Obama. Sote tujenge taifa letu na ni wakati wa wadau wa mchezo wa kikapu, kuongeza maarifa zaidi ya maendeleo.

Photos