VodaCom

Tangaza na gazeti la Bingwa.

NMB babu kubwa

Tangaza hapa huduma zako.

Commercial Bank of Africa

Tuna matumaini makubwa na huduma zako. Tangaza nasi.

AIRTEL huiweka dunia nzima karibu na watu

Haitoshi tu kusema AIRTEL YATOSHA. Inatosha kusema Airtel ni kila kitu.

TIGO, mtandao mkongwe zaidi nchini

TIGO ilionyesha njia. Sasa mawasiliano ni rahisi zaidi.

Sunday, August 4, 2013

Huruma ya kocha yaidhoofisha timu ya makanjanja



Timu ya taifa ya wasichana
KUCHELEWA kwa Bunge kupitisha Muswada wa Sheria ya Udhibiti wa Shughuli za Upangaji Nyumba na Makazi (Rental Housing Act), kunaipotezea Serikali mapato ya mabilioni ya fedha kuliko Sh 1000 ya kodi za kadi za simu (Simcard tax).

Akizungumza na MTANZANIA Jumatano, Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia, January Makamba, alisema ni vema sheria hiyo ikaanzishwa haraka ili kuondoa matatizo na lawama kuhusu kodi ndogo ndogo kama za kadi za simu zinazosumbua wananchi.

Makamba, alisema Wizara yake siyo iliyopanga tozo ya kodi hiyo kama baadhi ya wananchi wanavyodhani, kwa sababu haihusiki na kodi ya aina yoyote.

“Sheria ya udhibiti wa shughuli za upangaji, inatakiwa ije haraka kwani ndiyo hasa inayomnyonya mwananchi, kama unafanya kazi na unalipwa mshahara kwa mwezi, kwa nini ulipe kodi ya mwaka mzima, fedha ambayo haiendani na kipato.

“Kenya wanayo sheria hii ambapo mtu ana uwezo wa kulipia nyumba kwa miezi mitatu, kimataifa ni miezi miwili ambapo mtu analipia mwezi wa kwanza na wa mwisho.

“Sheria hii pia itasaidia kuanzishwa kwa mamlaka ya udhibiti wa nyumba kama ilivyo kwenye usafirishaji, ambako kuna Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), kwenye Nishati kuna EWURA, Chakula na Dawa kuna TFDA,” alisema.

Alisema malipo ya kodi ya nyumba kwa mwaka, ndiyo chanzo cha mtu kufanya maovu mengi kama kupokea rushwa, kujiingiza katika biashara ya dawa za kulevya, wizi na mengineyo.

Aidha, Makamba amesema Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, ni mnafiki kwa kukimbilia kutoa namba yake ya simu ya mkononi katika mkutano wa hadhara na kuandika kwenye mitandao, ili wananchi wampigie kumhoji kuhusu uwepo wa kodi kadi za simu wakati yeye mwenyewe alikuwepo bungeni kuipitisha.

“Mnyika ni mnafiki, yeye alikuwepo bungeni na alilijua fika suala hili wala hakusema kitu, baada ya kusikia watu wanalalamika ndiyo anaanza kuongea ongea.

“Ukiona mtu anafanya siasa nje ya Bunge ujue anatafuta umaarufu, kanuni zinamruhusu Mbunge yeyote kupeleka sheria ya mabadiliko, namna ya kubadilisha sheria sio kutoa namba za simu za watu, hizo ni siasa uchwara.

“Rais alishalitolea maamuzi na Serikali inalishughulikia, watu wasiwasikilize wanasiasa uchwara, wananchi wawe na subira kuhusu suala hili,” alisema Makamba.

Julai mwaka huu katika kikao chake cha bajeti, Bunge lilipitisha sheria ya kodi ya tozo ya kadi ya simu ya Sh 1000 kwa kila laini ya simu ya mkononi kwa mwezi, kodi ambayo imelalamikiwa na wananchi kuwa ni kubwa.

Hata hivyo, Rais Jakaya Kikwete, ameingilia kati suala hilo ambapo ameziagiza Wizara za Serikali zinazohusika na kodi na mawasiliano pamoja na kampuni za simu za mikononi nchini, kukutana mara moja kutafuta jinsi gani ya kumaliza mvutano wa kodi mpya ya kadi za simu hizo za mikononi.

Soka la Tanzania lapaa juu ya dari

Uwanja wa Sinza ukiwa katika hatua za mwisho

KUCHELEWA kwa Bunge kupitisha Muswada wa Sheria ya Udhibiti wa Shughuli za Upangaji Nyumba na Makazi (Rental Housing Act), kunaipotezea Serikali mapato ya mabilioni ya fedha kuliko Sh 1000 ya kodi za kadi za simu (Simcard tax).

Akizungumza na MTANZANIA Jumatano, Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia, January Makamba, alisema ni vema sheria hiyo ikaanzishwa haraka ili kuondoa matatizo na lawama kuhusu kodi ndogo ndogo kama za kadi za simu zinazosumbua wananchi.

Makamba, alisema Wizara yake siyo iliyopanga tozo ya kodi hiyo kama baadhi ya wananchi wanavyodhani, kwa sababu haihusiki na kodi ya aina yoyote.

“Sheria ya udhibiti wa shughuli za upangaji, inatakiwa ije haraka kwani ndiyo hasa inayomnyonya mwananchi, kama unafanya kazi na unalipwa mshahara kwa mwezi, kwa nini ulipe kodi ya mwaka mzima, fedha ambayo haiendani na kipato.

“Kenya wanayo sheria hii ambapo mtu ana uwezo wa kulipia nyumba kwa miezi mitatu, kimataifa ni miezi miwili ambapo mtu analipia mwezi wa kwanza na wa mwisho.

“Sheria hii pia itasaidia kuanzishwa kwa mamlaka ya udhibiti wa nyumba kama ilivyo kwenye usafirishaji, ambako kuna Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), kwenye Nishati kuna EWURA, Chakula na Dawa kuna TFDA,” alisema.

Alisema malipo ya kodi ya nyumba kwa mwaka, ndiyo chanzo cha mtu kufanya maovu mengi kama kupokea rushwa, kujiingiza katika biashara ya dawa za kulevya, wizi na mengineyo.

Aidha, Makamba amesema Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, ni mnafiki kwa kukimbilia kutoa namba yake ya simu ya mkononi katika mkutano wa hadhara na kuandika kwenye mitandao, ili wananchi wampigie kumhoji kuhusu uwepo wa kodi kadi za simu wakati yeye mwenyewe alikuwepo bungeni kuipitisha.

“Mnyika ni mnafiki, yeye alikuwepo bungeni na alilijua fika suala hili wala hakusema kitu, baada ya kusikia watu wanalalamika ndiyo anaanza kuongea ongea.

“Ukiona mtu anafanya siasa nje ya Bunge ujue anatafuta umaarufu, kanuni zinamruhusu Mbunge yeyote kupeleka sheria ya mabadiliko, namna ya kubadilisha sheria sio kutoa namba za simu za watu, hizo ni siasa uchwara.

“Rais alishalitolea maamuzi na Serikali inalishughulikia, watu wasiwasikilize wanasiasa uchwara, wananchi wawe na subira kuhusu suala hili,” alisema Makamba.

Julai mwaka huu katika kikao chake cha bajeti, Bunge lilipitisha sheria ya kodi ya tozo ya kadi ya simu ya Sh 1000 kwa kila laini ya simu ya mkononi kwa mwezi, kodi ambayo imelalamikiwa na wananchi kuwa ni kubwa.

Hata hivyo, Rais Jakaya Kikwete, ameingilia kati suala hilo ambapo ameziagiza Wizara za Serikali zinazohusika na kodi na mawasiliano pamoja na kampuni za simu za mikononi nchini, kukutana mara moja kutafuta jinsi gani ya kumaliza mvutano wa kodi mpya ya kadi za simu hizo za mikononi.

Utata mafuta ya ubuyu

Vita ya uwanjani imetimia

NA GABRIEL MUSHI
SIKU moja baada ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, kutoa tamko linaloeleza kuwa mafuta ya ubuyu hayana madhara katika mwili wa binadamu yakitumiwa vizuri, Serikali imekanusha hilo kwa kuwaonya wananchi wasiyatumie kwa sababu ni hatari.

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, jana alitangaza kuwa mafuta hayo si salama na kusisitiza kuwa huo ndiyo msimamo wa Serikali kuhusu mafuta hayo, hivyo wananchi waamue wenyewe kuyatumia au kutoyatumia.

Dk. Rashid alitoa kauli hiyo wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari baada ya kufungua semina ya siku mbili, iliyoandaliwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA) na Shirika la Afya Duniani (WHO).

Alisema kwa kuwa tayari TFDA imeshatoa tamko kuwa mafuta hayo si salama, hivyo wananchi ni hiari yao kutekeleza agizo hilo au kutolitekeleza.

“Tayari chombo cha serikali ambacho kina mamlaka juu ya hili kimeshatoa tamko, hivyo ni hiari ya wananchi kuamua wenyewe kuyatumia au kutoyatumia.

“Kwa sababu ni sawa na sigara, tumesema kabisa sigara inasababisha saratani na matatizo mengine tukaweka na onyo kwenye kasha la sigara zenyewe, hivyo ni hiari kutumia au kutotumia.

Alisema madhara yaliyo kwenye mafuta ya ubuyu yamegundulika hivi karibuni, baada ya kufanyiwa uchunguzi ambao ulichukua muda mrefu na hivyo kuchelewa kutangaza madhara yake.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Dk. Rashid, Mkurugenzi Mtendaji wa TFDA, Hiiti Sillo, alisema semina hiyo inashirikisha nchi 16 zilizopo kusini mwa Jangwa la Sahara.

Alisema imeandaliwa kwa ajili ya kuwapatia wakaguzi mbinu mpya za kudhibiti dawa bandia ambazo zinasababisha madhara kwa binadamu.

“Tatizo la dawa bandia linatakiwa kushirikiana na nchi nyingine, ndiyo maana mafunzo haya yatatumika kujenga uhusiano pamoja na kubadilisha uzoefu namna ya kukamata dawa hizo,” alisema.

Mwakilishi wa Shirika la Afya kutoka Geneva, Dk. Michael Deats, alisema tatizo la dawa bandia ni tatizo sugu linalozisumbua nchi za Bara la Afrika.

Hivi karibuni, TFDA ilipiga marufuku matumizi ya mafuta ya ubuyu kwa madai kuwa yanasababisha saratani, tamko ambalo lilipingwa vikali na wataalamu wa tiba mbadala.

Pamoja na hilo, juzi Taasisi ya Saratani ya Ocean Road  ilitangaza kuwa mafuta hayo ni salama iwapo yakitumiwa vizuri, tamko hilo pamoja na mwendelezo wa malalamiko kutoka kwa wananchi na wataalamu mbalimbali, limekuwa likizua utata kwa kuwa kila upande unaonekana kutoa msimamo wake jambo ambalo limeibua mjadala katika jamii.

Wabunge wagombea Sh milioni 1

Wakongwe wakijiandaa kwa kabumbu

NA JOHN MADUHU, MWANZA
WABUNGE wawili wa Kanda ya Ziwa, wameingia katika mzozo wa kugombea shilingi milioni moja.
Wabunge hao ni Lameck Airo wa Jimbo la Rorya mkoani Mara (CCM) na Ezekiel Wenje wa Jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza.

Akizungumza na MTANZANIA Jumatano jana kuhusu chanzo cha mzozo huo, Airo alisema anamtaka Wenje amrejeshee Sh milioni moja, alizompatia kwa ajili ya harambee ya kuchangia Shule ya Msingi ya Buchili wilayani Rorya, kwa sababu amezitumia badala ya kwenda kutoa mchango.

Airo alisema Wenje alikwenda kumuomba Sh milioni 5 mwishoni mwa wiki iliyopita alizodai kuwa ni mchango kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Buchili pamoja na ununuzi wa madawati na kumtaka ahudhurie harambee hiyo, lakini ratiba yake haikumruhusu hivyo alimpatia Sh milioni 1 ya mchango.

Alisema alishangazwa na taarifa alizopata kutoka kwenye harambee hiyo, kuwa Wenje hakutoa mchango aliompatia na badala yake alitoa maneno ya kashfa dhidi yake pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rorya, Charles Ochere, ambaye naye alimchangia kiasi cha Sh 500,000.

Alilalamika kuwa kitendo cha Wenje kutafuna fedha zake ni cha kihuni na kumtaka azirejeshe huku akimtahadharisha kuacha kumchafua katika majukwaa na badala yake washindane katika kuwaletea maendeleo wananchi.

“Nimempatia fedha kwa ajili ya harambee kiasi cha Sh milioni moja na Mwenyekiti naye alitoa Sh 500,000, kwanini hakutangaza mchango wetu katika harambee hiyo na badala yake yeye binafsi alitoa milioni moja pekee bila kutaja tulizompatia, inatia aibu kwa Mbunge kuchukua fedha kwa wabunge wenzako bila kuzifikisha kunakohitajika, kama alikuwa anataka kuongezea mtaji kwa ajili ya duka lake la madawa ni afadhali angetueleza,” alisema Airo.

Aidha Airo alieleza kusikitishwa na kauli iliyotolewa na Mbunge huyo katika harambee hiyo, kuwa amekuwa akimsaidia mambo kadhaa wakiwa bungeni mjini Dodoma na kueleza kuwa huo ni uongo.

Alipotafutwa Wenje kupitia simu yake ya kiganjani kuzungumzia tuhuma hizo, iliita bila kupokelewa.

Saturday, August 3, 2013

Hasheem Thabiti: Balozi wa kikapu nchini aliyekumbukwa na Obama

Na Markus Mpangala, Dar es Salaam
Hasheem alipokuja nchini mwake hivi karibuni
DIKEMBE Mutombo ni jina maarufu sana Afrika na duniani kote, kutokana na uwezo wake wa kucheza kikapu. Lakini jina lake kamili ni Dikembe Mutombo Mpolondo Mukamba Jean-Jacques Wamutombo.

Nyota huyo ana sifa kubwa kutokana na alivyoweza kusaidia ukuzaji wa mchezo huo, katika bara la Afrika hususani nchini mwake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mutombo kama anavyofahamika, alikuwa akicheza Ligi ya kulipwa ya Kikapu nchini Marekani, kwenye timu ya Houston Rockets. Kwa bara la Afrika mchezo wa Kikapu unapendwa zaidi kwenye nchi za Angola, Morocco na Nigeria pamoja na Tanzania, ambazo kwa nyakati tofauti zimekuwa na ufanisi kwa wachezaji wake.

Tunamkumbuka Mutombo kama tunavyofanya kwa Hasheem Thabiti, ambaye amekuwa akicheza Ligi ya Kulipwa ya Kikapu katika timu ya Oklahoma City Thunder ya Marekani.

Watanzania tunatakiwa kujivunia nyota huyo, ambaye amekuwa na mchango mkubwa wa maendeleo ya mchezo wa kikapu hapa nchini na kuonyesha kila dalili za kufuata nyayo za Dikembe Mutombo, ambaye aliisaidia sana nchi yake.

Bahati nzuri pia, ziara ya Rais Barack Obama, imefungua masikio ya wengi kuwa anatambua kuwa tunaye mchezaji mahiri nchini mwake. Katika mazungumzo yake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Rais Obama alisema kuwa anatambua kuwa nchi yetu inaye mchezaji kikapu, na hivyo kufanya mazungumzo ya kipekee na mwenyeji wake Rais Kikwete.

Kwa namna nyingine, kauli ya Rais Obama inatukumbusha kuwa kuna uwezekano mkubwa sana, sekta ya michezo hususani mchezo wa kikapu ikanufaika zaidi na matembezi yake ya kikazi.

Tunakumbuka kuwa klabu ya Seattle Sounder ya Marekani, ilimchukua winga Mrisho Ngassa wakati akichezea Azam, ili kufanya majaribio klabuni hapo.

Tuliona Ngassa akicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Manchester United. Tunafahamu kuwa Seattle Sounders iliingia ubia na klabu ya African Lyon ya hapa nchini, ili kuendeleza michezo, huku Azam nayo ikiwa mshirika mzuri.

Ziara ya Obama ambayo inamkumbuka nyota wetu Hasheem Thabiti, bila shaka inafungua milango zaidi kwa wachezaji wa mpira wa kikapu na sekta ya michezo kwa ujumla.

Rais Kikwete amekuwa na juhudi za kuendeleza michezo, tangu nia ya kuialika klabu ya Real Madrid, pamoja na mikakati ya sasa ya kuanzishwa akademi ambayo itaishirikisha klabu ya Sunderland ya England.

Ziara ya Obama na kutajwa kwa Hasheem Thabiti, kuna maana moja kuwa rais huyo anatambua kuwa Tanzania imejaliwa vipaji, ndiyo maana mchezaji huyo amekuwa miongoni mwa nyota waliosajiliwa na timu ya kulipwa za ligi ya NBA nchini Marekani.

Kuna kitu kimoja muhimu cha kukiangalia hapa, Obama ametembelea mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Symbion, ambayo ni mshirika wa klabu ya Sunderland.

Kwa maana hiyo ushirika huo kwa wanamichezo, utaleta manufaa makubwa, kwani kwenye mazungumzo yake Rais Obama ameeleza kutambua umuhimu wa Thabiti.

Bila shaka, juhudi zilizofanywa na Thabiti katika kuendeleza mchezo huu, na kwa kuwa alishawahi kukutana na Rais Kikwete mara kadhaa, sasa nyongeza itakuwepo na sekta ya michezo itapata mwamko mpya.

Ni rahisi kutumia ziara hii kuanzisha ushirikiano wa Sunderland, Symbion na Oklahoma City Thunder, ili kuupa kipaumbele mchezo wa kikapu kote nchini, ikiwezekana zaidi ya kipindi cha utawala wa Jackson Kalikumtima.

Tunafahamu tangu kuondoka kwa Jackson Kalikumtima, mchezo wa kikapu haukuwahi kupiga hatua kubwa, lakini kwa ziara ya Rais Obama, ni muhimu kwa wadau wa mchezo huo kusaka njia mbadala ya kuboresha zaidi.

Kwa hakika Thabiti ni balozi wetu wa mchezo wa kikapu, ambaye amekumbukwa na Rais Obama. Sote tujenge taifa letu na ni wakati wa wadau wa mchezo wa kikapu, kuongeza maarifa zaidi ya maendeleo.

Photos