Sunday, November 10, 2013

Benchi la ufundi Simba kuwasilisha ripoti wiki hii

NA EZEKIEL TENDWA

RIPOTI ya benchi ya ufundi la timu ya Simba, inatarajiwa kuwasilishwa kwa  kamati ya utendaji wiki hii.

Akizungumza jana, Ofisa habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema kuwa makocha wa timu hiyo wameahidi kuwasilisha ripoti kwa kamati ya utendaji wiki ili iweze kufanyiwa kazi.

Alisema kwamba baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania bara na timu yao kumaliza wakiwa nafasi ya nne, walitoa muda kwa benchi lao la ufundi kuandaa ripoti hiyo ambayo wataiwasilisha ndani ya wiki hii.

“Baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza, tulitoa muda kwa benchi letu la ufundi kuandaa ripoti yao na mapendekezo yao ambapo ndani ya wiki hii wataiwasilisha nasi tutaifanyia kazi,” alisema.

Alisema baada ya kupata ripoti hiyo, wataifanyia kazi kwani lengo lao ni kuhakikisha mzunguko wa pili timu hiyo inafanya vizuri na kujikita kileleni mwa msimamo ambao kwa sasa unakaliwa na watani zao wa jadi Yanga.

0 comments:

Post a Comment