Sunday, November 10, 2013

Azam, Coastal Union watunishiana misuli

NA ZAITUNI KIBWANA

TIMU za Azam na Coastal Union zinazoshiriki michuano ya Kombe la Uhai inayoshirikisha wachezaji wenye umri chini ya miaka 20 wa klabu za Ligi Kuu, wametunishiana misuli kwenye michezo ya ufunguzi wa mashindano hayo.

Ofisa habari wa Azam, Jafari Iddi aliliambia BINGWA kuwa kikosi chao kimeahidi ubingwa wa michuano hiyo, hivyo Coastal Union wajiandae kwa kichapo.

Wakati Jafari akiyasema hayo msemaji wa Coastal Union, Hafidhi Kido alisema kuwa mwaka huu wana vijana watakaoleta changamoto kwenye michuano hiyo.

Michuano hiyo mwaka huu itafanyika kwenye viwanja vya Karume na Azam Complex, Dar es Salaam.

Kundi A linaundwa na timu za Azam, Coastal Union, JKT Ruvu Stars, Mbeya City na Yanga, wakati kundi B ni Ashanti United, Mgambo Shooting, Oljoro JKT na Ruvu Shooting, Kagera Sugar, Mtibwa Sugar, Rhino Rangers na Tanzania Prisons ndizo zinazounda kundi C.

Kwa mujibu wa Ofisa Mashindano, Idd Mshangama, alisema kuwa mechi hizo za ufunguzi timu za Yanga na Mbeya City (saa 8 mchana- Karume).

Kundi B ni Ruvu Shooting na Ashanti United saa 4 asubuhi- Karume, Oljoro JKT na Simba saa 10 jioni- Karume

0 comments:

Post a Comment